Friday, May 15, 2026

Top Stories

View all
SERIKALI YATOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 11 KUJENGA MIRADI YA MAJI WILAYANI NYASA,MKUU WA MKOA AAGIZA WEZI WA VIFAA VYA UJENZI KUFIKISHWA MAHAKAMANI

SERIKALI YATOA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 11 KUJENGA MIRADI YA MAJI WILAYANI NYASA,MKUU WA MKOA AAGIZA WEZI WA VIFAA VYA UJENZI KUFIKISHWA MAHAKAMANI

Tenki la maji linalojengwa kupitia mradi wa maji katika kijiji cha Mwerampya wilayani Nyasa. Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas akikagua tenki la kuhifadhia maji  kupitia mradi wa maji utakao wanufaisha zaidi ya wakazi 26,477 wa vijiji  saba wilayani Nyasa. Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas kushoto,akimsalimia mkazi wa kijiji cha Mwerampya Maria Ngairo aliyetoa sehemu ya ardhi yake kwa ajili ya kujenga   tenki la maji kupitia mradi wa maji ambao utawanufaisha wakazi wa vijiji vitano katika wilaya ya Nyasa. ************************* Na Muhidin Amri, Nyasa MKUU  wa mkoa wa Ruvuma Kanal Laban Thomas,amemuagiza Kaimu Mkuu wa wilaya ya Nyasa Aziza Mangosongo kupitia kama ya ulinzi na usalama,kuwakamata na kuwafikisha mahakamani mafundi wa kampuni ya Emirate Builder Co Ltd waliohusika kuiba vifaa vya ujenzi wa miradi ya maji katika kijiji cha Lituhi na Liuli wilayani humo. Kanal Laban ametoa agizo hilo kwa nyakati tofauti, wakati alipotembelea ujenzi wa miradi miwili ya maji katika kijiji cha Mwerampya na Liuli wilayani Nyasa inayotekelezwa na Serikali kupitia wakala wa maji safi na  usafi wa mazingira(Ruwasa). Mkuu wa mkoa,amewataka wananchi kutambua kuwa miradi hiyo ni ya kwao,kwa hiyo wana wajibu wa kuilinda na kuepuka kununua vifaa vinavyoletwa kwa ajili ya ujenzi wa miradi kutoka kwa mafundi. Alisema,baadhi ya mafundi ndiyo wanaohusika  kuiba vifaa na kuwaomba wananchi kutokuwa sehemu ya watu wanaohujumu miradi hiyo kwani Serikali inatumia fedha nyingi kwa ajili ya kutatua changamoto na kuleta maendeleo. “hakuna maana  kama Mheshimiwa Rais Samia anaangaika usiku na mchana kutafuta fedha kwa ajili ya kuwaletea maendeleo wananchi,alafu sisi  ndiyo tunakuwa wa kwanza kuiba vifaa vinavyoletwa,tabia hii haikubailiki hata kidogo,nawaomba wananchi  kushirikiana na serikali yenu kuwafichua watu wanaojihusisha na tabia hiyo”alisema Kanal Laban. Aidha,amemtaka Mkandarasi kampuni ya Emirate Builders Co Ltd, kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha kazi hiyo kwani wananchi wana hamu kubwa ya kupata  maji safi na salama ili waweze kuyatumia katika shughuli zao za maendeleo. Kwa upande wake Meneja wa Ruwasa wilaya ya Nyasa  Jeremia Maduhu alisema,Serikali imetoa Sh.bilioni 11,718,087.448 kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ya maji katika kijiji cha Lituhi na Liuli wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma. Maduhu alieleza kuwa, miradi yote miwili  inajengwa na kampuni ya Emarate Builders Co Ltd na iko katika hatua mbalimbali za utekelezaji wake huku akibainisha kuwa kati ya fedha hizo Sh.bilioni 6,595,019,723 zitatumika kutekeleza mradi wa maji Lituhi  ambapo mkandarasi ameshalipwa shilingi milioni 989,252,958.50. Kwa mujibu wa Maduhu,mradi  huo utakapokamilika utahudumia vijiji saba vya Lituhi,Kihuru,Nkaya,Mwera mpya, Ndumbi Liweta na Mbaha vyenye takribani wakazi 26,477. Alisema,katika mradi huo kazi zilizopangwa kufanyika ni ujenzi wa tanki la la kuhifadhia maji la lenye mita za ujazo 500, kujenga vituo 19 vya kuchotea maji, ujenzi wa chanzo,ununuzi wa bomba za urefu wa mita 77.570,kuchimba mitaro na ujenzi wa ofisi ya chombo cha watumia maji. Alitaja kazi zilizoanza kufanyika ni  ujenzi wa chanzo, ujenzi wa tenki la kuhifadhia maji la lita 500,000 na ununuzi wa mabomba. Akizungumzi mradi wa maji Liuli alisema,mradi  huo umetengewa jumla ya Sh.bilioni 4,718,087,448 na utahudumia vijiji vitano vya Liuli,Nkalachi,Hongi,Puulu na Mkali A na B na utawanufaisha zaidi ya wakazi 25,808. Baadhi ya wananchi wameiomba Serikali kuharakisha ujenzi wa mradi huo ili kuwanusuru na adha ya kuamka usiku wa manane kwenda kutafuta maji kwa ajili ya matumizi yao ya kila siku. Maria Ngailo mkazi wa kijiji cha Mwerampya kata ya Lituhi alisema,tatizo la maji katika kijiji hicho limesababisha hata baadhi ya wanafunzi kukatisha masomo kwa kupata mimba  wanapokwenda kutafuta maji mbali na makazi yao.

TAMISEMI YATAMBA KUFANYA VIZURI BAISKELI

TAMISEMI YATAMBA KUFANYA VIZURI BAISKELI

Na Asila Twaha, Tanga TIMU ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI ya baiskeli kesho inaingia uwanjani katika Mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara…