Na Happy Lazaro,Arusha .
Amesema kuwa kampuni hiyo ni miongoni mwa wadhamini wa Kilimanjaro Summit Challenge, programu maalum inayowapa washiriki wa KiliFair fursa ya kushiriki safari ya kupanda Mlima Kilimanjaro na kujionea vivutio vya kipekee vinavyopatikana nchini Tanzania.
Nacy amesema kuwa ,ushiriki wa kampuni hiyo katika Kilimanjaro Summit Challenge umechangia kwa kiasi kikubwa kuitangaza Tanzania kimataifa kupitia utalii wa mlima, michezo ya nje na kuimarisha ushirikiano kati ya wadau wa sekta ya utalii duniani.
Nacy amesema kuwa Zara Adventures Tours Tanzania, kama mmoja wa wadau na washiriki wa maonyesho hayo, imeridhishwa na maandalizi na uendeshaji wa KiliFair 2026 ambao umewezesha kuwakutanisha wadau wa utalii kutoka Tanzania na mataifa mbalimbali duniani.
“Tumefurahi kuona wageni na washiriki kutoka mataifa mbalimbali wakifika nchini Tanzania kushiriki maonyesho haya sambamba na kupata fursa ya kutembelea banda letu na kuweza kujua huduma tunazotoa kwa ajili ya ushirikiano zaidi.”amesema .
Aidha, ametoa pongezi kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa juhudi kubwa zinazoendelea kufanyika katika kuimarisha na kutangaza utalii wa Tanzania katika soko la kimataifa.
“Tunaendelea kushuhudia matokeo chanya ya juhudi hizi. Idadi ya watalii wanaofika nchini inaongezeka, na matukio makubwa kama KiliFair yanafungua fursa zaidi za biashara, uwekezaji na ushirikiano katika sekta ya utalii,” ameongeza .
Aidha Nacy amewashukuru waandaaji wa KiliFair 2026, washirika, wadhamini na wadau wote waliofanikisha maonyesho hayo pamoja na Kilimanjaro Summit Challenge, akieleza kuwa ushirikiano huo umechangia kuimarisha taswira ya Tanzania kama moja ya nchi bora za utalii duniani.
Amesema kampuni hiyo itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuendeleza utalii endelevu na kuitangaza Tanzania kama kitovu cha vivutio vya utalii barani Afrika na duniani kwa ujumla.




