
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Jumatano, Septemba 09, 2026, ameshiriki Hitma ya kumuombea marehemu Hafidh Amir Hassan, aliyekuwa mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Hitma hiyo imefanyika Kizimkazi Mkunguni, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar, ikiwakutanisha viongozi mbalimbali, ndugu, jamaa na waombolezaji kwa ajili ya kumuombea marehemu.
