Kamishna Msaidizi wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bi. Emma Komba, akizungumza wakati wa kufunga kwa niaba ya Kaimu Kamishna wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma, Wizara ya Fedha, Bw. Alex Habara, kikao kazi cha Mapitio ya Sheria ya Ununuzi wa Umma Sura ya 410, kikao kazi kilichowakutanisha watekelezaji wa ununuzi wa umma na ugavi katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na vituo vya afya.

Washiriki wa kikao kazi, kilichowakutanisha watekelezaji wa ununuzi wa umma na ugavi katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na vituo vya afya, wakifuatilia kikao hicho, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper, Jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Sheria kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma, Bw. Paul Kadushi, akizungumza wakati wa kikao kazi, kilichowakutanisha watekelezaji wa ununuzi wa umma na ugavi katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na vituo vya afya, wakifuatilia kikao hicho, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper, Jijini Dodoma.

Kamishna Msaidizi wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma – Wizara ya Fedha, Bi. Emma Komba (katikati walioketi), Mkurugenzi wa Sheria kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma, Bw. Paul Kadushi (kulia kwake), Afisa Sheria Daraja la Kwanza, Wizara ya Fedha, Bw. Paul Kimweri (kushoto kwake), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa kikao kazi, kilichowakutanisha watekelezaji wa ununuzi wa umma na ugavi katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na vituo vya afya, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper, Jijini Dodoma.

Kamishna Msaidizi wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma – Wizara ya Fedha, Bi. Emma Komba, akiagana na Mkurugenzi wa Sheria kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma, Bw. Paul Kadushi, baada ya kufunga kikao kazi, kilichowakutanisha watekelezaji wa ununuzi wa umma na ugavi katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na vituo vya afya, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper, Jijini Dodoma.

Katibu wa Afya kutoka Kituo cha Afya Nkuhungu, Bi. Patricia Joseph, akitoa maoni wakati wa Kikao kazi kilichoandaliwa na Wizara ya Fedha, cha Mapitio ya Sheria ya Ununuzi wa Umma Sura ya 410, kilichowakutanisha, Watumishi wa Idara hiyo, Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) pamoja na watekelezaji wa Ununuzi wa Umma katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi, Sekondari, na vituo vya afya, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper, Jijini Dodoma.

kikao kazi, kilichowakutanisha watekelezaji wa ununuzi wa umma na ugavi katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na vituo vya afya, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper, Jijini Dodoma. (Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF – Dodoma)

Na Asia Singano, WF – Dodoma
Wizara ya Fedha, imeendelea kupitia upya Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, kwa lengo la kuioanisha na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, kupitia kikao kazi kilichowakutanisha watelekezaji wa ununuzi wa umma na ugavi katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na vituo vya afya.
Mchakato huo ulianza kwa kikao kazi kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa St. Gasper, Jijini Dodoma, ambapo watekelezaji wa Ununuzi wa Umma katika ngazi za chini za Serikali za Mitaa, Shule za Msingi na Sekondari pamoja na vituo vya afya, walipata fursa ya kutoa maoni na mapendekezo yatakayosaidia kuboresha Sheria hiyo.

Akizungumza wakati wa kufunga Kikao hicho, Kwa niaba ya Kaimu Kamishna wa Idara ya Sera za Ununuzi wa Umma – Wizara ya Fedha, Bw. Alex J. Habara, Kamishna Msaidizi wa Idara hiyo Bi. Emma Komba, alisema mapitio hayo yanalenga kujenga mfumo wa kisasa unaojumuisha hatua zote za mnyororo wa ugavi, kuanzia upangaji wa mahitaji, ununuzi, ugomboaji wa mizigo, upokeaji, uhifadhi na utunzaji, usambazaji, hadi uondoshaji wa mali za umma.

Aliongeza kuwa mapitio hayo pia yamezingatia nguzo na malengo ya Dira ya Maendeleo 2050, ikiwemo ukuaji wa uchumi, maendeleo ya viwanda, pamoja na maendeleo jumuishi na endelevu.

‘’Mapitio ya Sheria hii ni hatua ya kimkakati ya kuhakikisha kuwa masuala yote yanayohusu mnyororo mzima wa ugavi yanajumuishwa kikamilifu katika Sheria mpya, na kwamba mageuzi hayo yatakuwa chachu ya kuchochea maendeleo ya Taifa’’ alisema Bi. Emma.

Aliongeza kuwa Wizara ya Fedha, itazingatia na kufanyia kazi mapendekezo yote yaliyowasilishwa kwa kuyachambua kwa kina ili kubaini maeneo ya kuboresha na kuweka misingi imara itakayosaidia Taifa kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo 2050.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Sheria kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA), Bw. Paul Kadushi, alisisitiza kuwa Mamlaka hiyo itaendelea kutoa elimu kwa watekelezaji wote wa ununuzi wa umma na ugavi ili kurahisisha utendaji kazi katika Mfumo wa Kielektroniki wa Ununuzi wa Umma (NeST).

‘’Sisi PPRA kama wadhibiti wa ununuzi wa umma, sehemu ya nguvu ambayo tumeelekeza kwenye kutoa elimu kwa wazabuni na makundi maalumu, tunahitaji pia kuelekeza kwenu na kuwajengea uwezo ili muweze kutekeleza kazi za ununuzi wa umma kwa ufanisi zaidi’’ alisema Bw. Kadushi.

Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura ya 410, imeipa Wizara ya Fedha, jukumu la kisheria la kupitia na kuhuisha sera, sheria, kanuni, miongozo, pamoja na maelekezo mbalimbali yanayohusu ununuzi wa umma na ugavi nchini.