“Kwa kweli sisi kama wanawake wa UWT kata ya Pangani tunapenda kumshukuru kwa dhati Mwenyekiti wetu wa Wilaya mama yeetu Elina Mgonja kwa kuweza kuamua kutekeleza ahadi yake kwa vitendo ya kuja kututembelea katika Kata yatu na haya mafunzo yataweza kutusaidia kwa kiasi kikubwa wanawake kuweza kujikwamuaa kiuchumi,”amebainisha Mwenyekiti huyo.
Mwenyekiti huyo amesema kwamba fursa za kupatiwa mafunzo hayo itakuwa ni moja ya mkombozi mkubwa ya kuweza kujifunza mbinu na ujuzi mbali mbali wa namna ya kuweza kujifunza namna ya kutengeneza bidhaa hizo ambazo zitaweza kuwasaidia kuondokana na wimbi la umasikini na kuleta chachu ya maendeleo.
Naye mmoja wa wananawake wajasiriamali kutoka kata ya Pangani Rehema Seleman ambaye ameweza kunufaika kwa kiasi kikubwa na mafunzo ambayo alipatiwa na Mwenyekiti huyo wa UWT Wilaya ya Kibaha katika kipindi cha nyuma hakusita kueleza mafanikio ambayo ameweza kuyapata ikiwemo suala la kuanzisha miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwemo kuwepo na kujenga makazi ya kuishi kupitia shughuli za ujasiriamali.
“Mimi niliweza kupata fursa ya mafunzo mbali mbali kutoka kwa Mwenyekiti wetu wa Jumuiya ya wanawake wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini na leo hii nashukuru nimepata mafanikio makubwa sana ikiwemo nimeweza kujenga nyumba yangu na mambo mengine mbali mbali nimefanya ya kimaendeleo kwa hiyo mwalimu wangu Elina Mgonja ameweza kunitoa mbali sana katika kunipa ujuzi na maharifa,”amebainisha Rehema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja amesema kwamba ameamua kufanya ziara hiyo ya kuweza kutoa mafunzo hayo ya ujasiriamali kwa wanawake wote wa UWT kutoka kata zote 14 zilizopo katika Halmashauri ya manispaa ya Kibaha.
