Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga SC, wamefanikiwa kuvuna pointi tatu katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo uliopigwa leo, Agosti 24, 2026, katika Dimba la KMC Mwenge, Dar es Salaam.

Kufuatia ushindi huo, Yanga SC imefikisha pointi tisa baada ya kucheza michezo mitatu, na kupanda hadi nafasi ya kwanza katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Yanga SC inalingana kwa pointi na Simba SC, lakini imepanda kileleni kutokana na kuwa na tofauti nzuri ya mabao ya kufunga na kufungwa.