Wekundu wa Msimbazi, Simba SC, wametoka sare ya bila kufungana (0-0) dhidi ya Jamus SSFC katika mchezo wa hatua ya makundi wa michuano ya Kagame Cup 2026.

Hii ni sare ya pili mfululizo kwa Simba SC katika mashindano hayo, baada ya awali kutoka sare dhidi ya Mogadishu City FC.

Katika mchezo wao wa mwisho wa hatua ya makundi, Simba SC itavaana na Singida BS. Ushindi katika mchezo huo ni muhimu kwa Wekundu wa Msimbazi ili kufufua matumaini ya kufuzu hatua inayofuata ya mashindano.