Na. Fullshangwe Blog, Updates Michezo
Timu za Ufaransa na Norway zimehitimisha hatua ya makundi ya Kombe la Dunia 2026 kwa kufuzu kwenda hatua ya 32 bora, baada ya kumaliza nafasi mbili za juu katika Kundi I.
Ufaransa iliendeleza ubabe wake kwa kuichapa Norway mabao 4-1 katika mchezo uliochezwa Juni 26, 2026, na kujihakikishia kumaliza hatua ya makundi ikiwa kinara wa kundi hilo kwa pointi 9.
Kwa upande wake, Senegal iliipiga Iraq mabao 5-0 katika mchezo mwingine wa Kundi I, ushindi uliowaongezea matumaini ya kusonga mbele kupitia nafasi ya timu bora zilizomaliza nafasi ya tatu, huku Iraq ikitolewa rasmi kwenye mashindano.
Baada ya kukamilika kwa michezo hiyo, Ufaransa na Norway zimesonga mbele hatua ya 32 bora,
