Na Victor Masangu, Pwani

Mamlaka ya  mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Pwani katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka  30 imeamua  kurudisha fadhila kwa jamii pamoja na walipa kodi   kwa kufanya usafi katika stendi ya mabasi chalinze pamoja na  kutoa vifaa  mbali mbali  vya usafi kwa wafanyabiashara  pamoja na kutoa vyombo  mbali mbali  vya kupikia kwa wakinamama ambao ni mama lishe.

Katika msafara huo ambao uliongozwa na Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Mapato (TRA) Zanzibar Salehe Haji Pandu amesema kwamba wameamua kwenda kuwatembelea wafanyabiashara wa chalinze kwa lengo la kuweza kuwasaidia ili waweze  kuhakikisha wanapiga hatua  katika kutimiza ndoto zao.

“Katika kuelekea katika maadhimisho ya miaka 30 ya TRA tumeamua kwenda kufanya usafi katika  stendi ya Chalinze ikiwa pamoja  kugawa vifaa vya Usafi pamoja na Vyombo vya kupikia kwa Mama lishe pamoja na  kuwawatembelea wafanyabiashara wa stendi ya Chalinze katika kutambua mchango wao  kwa walipa kodi,”amebainisha Kamishna Haji.

Aidha Naibu Kamisha huyo  amebainisha kwamba  Mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kiasi kikubwa inawategemea Wafanyabiashara hivyo ni muhimu kuhakikisha wafanyabiashara wanakua huku nguvu kubwa wakielekeza kwa wafanyabiashara walio nje ya wigo Kodi ili kuongeza idadi ya Walipakodi wengine Wapya.

Kwa upande wake  Meneja wa TRA Mkoa wa Pwani Peter Eliona amessema kwamba wataendelea kushirikiana bega  kwa bega na na wafanyabiashara wote na kuwahimiza kuweka misingi ya kuweza kulipa kodi kwa wakati kwa lengo la kuiwezesha serikali kupata mapato yao.

Meneja Eliona amebainisha kwamba wameona kuna  umuhimu mkubwa wa kwenda katika stendi hiyo ya mabasi chalinz e na kupata  fursa ya kuzungumza na wafanyabiashara ikiwa pamoja na kufanya matendoya kugawa mahitaji mbali mbali ambayo yatawasaidia katika suala zima la utekelezaji wa majukumu yao ikiwemo mama lishe pamoja na wafanyabiashara.

Naye Meneja wa Stendi ya Chalinze Henry Mwalugenge akizungumnza kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Chalinze  amewashukuru TRA Mkoa wa Pwani kwa kutoa elimu ya Mlipakodi katika eneo hilo pamoja Vifaa vya Usafi ikiwani  mojawapo ya kutengeneza mahusiano mazuri na Walipakodi.

Aidha Diwani wa Kata ya Bwilingu Laurence Peter amewapongeza TRA kwa kuvuka malengo ya ukusanyaji wa mapato na kurudisha kwa jamii itaongeza chachu ya Wafanyabishara kulipa kodi.

Akizungumnza kwa niaba ya Mama lishe Wa stendi ya mabasi chalinze,Mwenyekiti wa Mama lishe Bi.Zainabu Bakari amewashukuru TRA kwa kuwapa vifaa hivyo vitakavyo kwenda kuwarahisishia utendajikazi wao pamoja na kutengeneza mahusiano mazuri kwa walipa kodi.

Mamlaka ya mappato TRA Mkoa wa Pwani imeamua katika kuelekea maadhimisho ya miaka 30  imeamua kufanya mambo mbali mbali ikiwemo kufanya kongamano kwa  walipa kodi na wadau, pamoja na kutembelea stendi ya mabasi chalinze na kugawa vifaa  kwa wafanyabiashara, na mama lishe sambamba na kutoa elimu kwa mlipa kodi.