Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti aina ya stafeli kama kumbukumbu ya uzinduzi wa Jengo la Tiba Mionzi (Radiotherapy Unit) katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC), Moshi mkoani Kilimanjaro tarehe 24 Juni, 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kuashiria uzinduzi wa Jengo la Tiba Mionzi (Radiotherapy Unit) katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro tarehe 24 Juni, 2026. Uzinduzi huu unaashiria hatua kubwa ya kuimarisha huduma za matibabu ya saratani nchini kwa kuongeza upatikanaji wa huduma za kisasa katika mikoa ya Kaskazini na Afrika Mashariki.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini (KCMC) ambaye pia ni Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk. Alex Gehaz Malasusa, kuashiria uzinduzi wa Jengo la Tiba Mionzi (Radiotherapy Unit) katika Hospitali ya KCMC, Moshi mkoani Kilimanjaro tarehe 24 Juni, 2026. Uzinduzi huu unaashiria hatua kubwa ya kuimarisha huduma za matibabu ya saratani nchini kwa kuongeza upatikanaji wa huduma za kisasa katika mikoa ya Kaskazini na Afrika Mashariki.