Na. Fullshangwe Blog, Updates Michezo
Hispania imeanza kampeni yake ya Kombe la Dunia 2026 kwa kutoka sare ya bila kufungana dhidi ya Cape Verde katika mchezo wa Kundi H uliochezwa leo Juni 15,2026.
Matokeo hayo yameifanya kila timu kujikusanyia pointi moja katika msimamo wa kundi hilo, ambalo pia linazijumuisha Saudi Arabia na Uruguay.
Baada ya mchezo huo, Hispania na Cape Verde zina pointi moja kila moja huku zikisubiri matokeo ya mchezo mwingine wa Kundi H kati ya Saudi Arabia na Uruguay ili kubaini msimamo kamili wa kundi hilo.
