Mabigwa Watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga SC wameibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu uliopigwa leo Machi 5, 2026 Mkoani Singida.
Mabao ya Yanga SC yamefungwa na dakika ya 39 Dube, dakika ya 45+2’ Okello (Pen) pamoja na Mudathir dakika ya 58 kipindi Cha pili.
Kwa matokeo haya, Yanga wanafikisha alama 32 kileleni mwa msimamo wa ligi, huku watani zao Simba SC wakiwa na alama 24 na mechi moja mkononi.
