Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na ujumbe wa Jukwaa la Mabunge la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR) ukiongozwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Domitien Ndayizeye, Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar, tarehe 26 Oktoba, 2025. FP-ICGLR ni miongoni mwa misheni mbalimbali zilizowasili nchini kwa ajili ya uangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa tarehe 29 Oktoba, 2025.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kiongozi wa Jukwaa la Mabunge la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR) Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Domitien Ndayizeye Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar, tarehe 26 Oktoba, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na ujumbe wa Jukwaa la Mabunge la Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR) ukiongozwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Burundi, Mhe. Domitien Ndayizeye, Ikulu ndogo Tunguu, Zanzibar, tarehe 26 Oktoba, 2025.



