Maelfu ya Wananchi wa Lamadi wilayani Busega mkoani Simiyu wakiwa pamoja na Viongozi mbalimbali wa Chama na Jumuiya, Viongozi wa Dini na Machifu kwa umoja wao wamempokea Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro leo tarehe 9 Oktoba 2025.
Pamoja na mambo mengine, Dkt. Migiro ametanguliza salamu za upendo na ujio wa Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Rais Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 ambaye pamoja na kuja kusalimia, atanadi ilani ya CCM, Sera na Ahadi zake na kuomba kuwa kwa mafiga matatu.