Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Begi lenye Fomu za kugombea nafasi ya Rais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele katika Ofisi za Tume hiyo Njedengwa Jijini Dodoma tarehe 09 Agosti, 2025. Kushoto ni Mgombea Mwenza Dkt. Emmanuel John Nchimbi
Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha Begi lenye Fomu zake za kugombea nafasi hiyo mara baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele katika Ofisi za Tume hiyo Njedengwa Jijini Dodoma tarehe 09 Agosti, 2025.

Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi wa Wilaya ya Chamwino waliojitokeza kumuunga mkono tarehe 09 Agosti, 2025 wakati akielekea katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) kwa ajili ya kuchukua Fomu ya kugombea nafasi ya Rais katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika 29 Oktoba, 2025. Pia wananchi hao walimchangia kiasi cha Shilingi Laki Mbili na Nusu ili zimsaidie kulipia fomu hiyo.




