Mkurugenzi wa kampuni ya kitalii ya Pamoja Afrika iliyopo Karatu,Asheri Kiisay akizungumza na wateja walipotembelea banda lao  kwa ajili ya kupata maelezo ya huduma wanazotoa.
…………..
Happy Lazaro, Arusha.
Watanzania wametakiwa kuwa na utamaduni wa kutembelea hifadhi za kitalii zinazotuzunguka ili kutangaza utalii wa ndani badala ya kuachia wageni kutoka nje kuja kutangaza utalii hapa kwetu.
Aidha amesema kuwa ,ni vizuri wakajenga utamaduni wa kuvienzi vya  kwetu kwani vivutio  mbalimbali vya utalii ni vya kwetu na vinatuhusu  sisi wenyewe ,hivyo ni lazima tujenge  utaratibu  wa kutembelea hifadhi mbalimbali na kutangaza vivutio vilivyopo. 
Hayo yamesemwa mkoani Arusha na Mkurugenzi wa kampuni ya kitalii ya Pamoja Afrika iliyopo Karatu,Asheri Kiisay ambapo  amesema wataendelea kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii katika nchi mbalimbali huku  lengo likiwa kumuunga mkono Rais Samia . 
Amesema kuwa, endapo sisi kama watanzania  tutajenga  utamaduni  wa kutembelea hifadhi mbalimbali itasaidia  sana sisi wenyewe kuwa mabalozi wazuri kwa ajili ya kutangaza vivutio hivyo na hivyo kuendelea kuwashawishi wafadhili mbalimbali kutembelea. 
Aidha amesema kuwa,kupitia kampuni hiyo wamekuwa wakitangaza  vivutio mbalimbali vya utalii kwa watalii wanaofika katika eneo hilo  kutokana na mandhari  nzuri iliyopo inayovutia na kuwafanya wengi wao kuendelea kufika eneo hilo.
Ameongeza  kuwa, watalii wanaweza kujionea  hoteli inayotembea kufuata wanyama wanaohama  kutoka Tanzania kwenda Masai Mara .
“Tanzania ni nchi nzuri sana na tumejionea namna ambavyo utalii umezidi kushika kasi baada ya Rais Samia kutangaza utalii kupitia filamu  yake ya The Royal Tour kwani ametusaidia sana kufungua nchi na kuturahisishia  kupata  watalii  wanaotoka  nchi mbalimbali kuja kujionea  vivutio  vyetu.”amesema .
Amesema kuwa,watalii wanapokuwa  kwenye hotel hiyo wanaweza kufanya utalii wakati wa usiku kwani ni mida  ambayo  unaweza kuona wanyama kwa karibu zaidi .
Aidha akizungumzia mafanikio makubwa waliyoyapata katika maonyesho hayo ambayo  hufanyika kila mwaka ni pamoja na kupata idadi kubwa ya wanunuzi wapya kwani kupitia  filamu ya The Royal Tour ya Rais Samia imesaidia sana watalii  kuendelea kufurika hapa nchini kwa ajili ya kujionea vivutio mbalimbali .
Hata hivyo amewataka watalii mbalimbali.ndani na nje ya nchi kujitokeza  kwa wingi katika katika maeneo hiyo ili waweze kujifunza maswala mbalimbali ya vitutio. 



                                
                             