Waziri wa Uchukuzi Mhe. Profesa Makame Mbarawa (katikati) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi na Maendeleo ya Miundombinu Nchini Zimbabwe Mhe. Mha. Joy Makumbe (wa pili kushoto ), wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ofisi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) Jijini Harare nchini Zimbabwe, tarehe 16 Oktoba, 2023.
Wengine katika picha ni Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe Mhe. Simon Sirro ( kushoto) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA Mha. Juma Kijavara ( kulia).