
Ng’ombe aina ya Sahiwal walioko Transamara nchini Kenya walioboreshwa kupitia Mradi wa Utafiti wa uboreshaji na utunzaji wa Mbari za ng’ombe unaofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la AU-IBAR.
Mratibu wa Mradi wa Sahiwal kutoka Tanzania, Dk. Zebron Nziku akimpongeza mfugaji wa ng’ombe wa Wilaya ya Kiligoris, Transmara nchini Kenya, Oltetia Ole Oltetia kutokana na juhudi kubwa alizofanya kuboresha mifugo yake.
Wafugaji wa Tanzania na Kenya wakijadiliana kwa pamoja namna bora kuboresha ufugaji wao wakiwa kwenye mafunzo katika Chuo cha Uchakataji Maziwa (DTI), Naivasha Kenya
Wafugaji wa Tanzania na Kenya walioko kwenye mafunzo nchini Kenya wakiwa katika picha ya pamoja na Mratibu wa Mradi wa Sahiwal , Dk Zebron Nziku na wataalamu wengine kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi mara baada ya kutembelea Chuo cha Uchakati Maziwa(DTI), Naivasha Kenya
Afisa Mtafiti wa Mifugo Mkuu (PLRO), Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Hassan Mruttu akisalimiana na mfugaji aliyeko kwenye mradi wa Sahiwal, Kantet Ole Kate wa Transmara Narok nchini Kenya mara baada ya wafugaji wa Tanzania kutembelea nchi hiyo kwa ziara ya mafunzo

Sign in to your account
