
Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) Kanda ya Ziwa Mashariki, Bi. Nuru Mwasulama akitoa taarifa fupi ya uanzishwaji wa Kanda hiyo itakayohudumia mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga na makao makuu yake yakiwa Bariadi Mjini, katika uzinduzi waa kanda hiyo uliofanyika Juni 20, 2019 Mjini Bariadi.



Kaimu Mganga mkuu wa Mkoa, Dkt. Mugune Maeka akitoa neno la shukrani mra baada ya kuhitishwa kwa uzinduzi wa Kanda ya Ziwa Mashariki ya Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) itakayohudumia mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga, Juni 20, 2019 Mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka (katikati mbele) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi, wataalam wa mkoa wa Simiyu na Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA) mara baada ya Uzinduzi wa Ofisi ya Mamlaka hiyo Kanda ya Ziwa Mashariki itakayohudumia mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga na makao makuu yake yakiwa Bariadi Mjini, Uzinduzi umefanyika Juni 20, 2019 Mjini Bariadi.
