Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya kwa kutambua mchango wa kipekee katika ubunifu na maendeleo ya sekta ya Nishati nchini ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa Shirika katika kuendeleza sekta hiyo.
Tuzo hiyo imekabidhiwa kwa Shirika la Umeme Tanzania TANESCO katika hafla ya tuzo za ujenzi wa miundombinu na uchimbaji madini kwa mwaka 2026, iliyofanyika Septemba 4, 2026 jijini Dar es Salaam.
Akikabidhi tuzo hiyo Mkurugenzi wa Usajili wa Wakandarasi Wizara ya Ujenzi Mhandisi Rhoben Nkori kwa Niaba ya Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega amelipongeza Shirika kwa kuendelea kuimalisha upatikanaji wa Umeme katika Maeneo mbalimbali hapa nchini Hali ambayo imekuwa Chachu ya kuchochea Maendeleo katika sekta mbalimbali hapa nchini.
Tuzo hiyo imetolewa na Chama cha Ujenzi na Miundombinu cha Tanzania (CCIT), ikiwa ni utambuzi wa mchango wa TANESCO katika ubunifu na maendeleo ya nishati nchini.
