Matukiokatikapicha

Kaimu Kamishna wa Ustawi wa Jamii Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Faithmary Lukindo akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo katika Kongamano la Maadimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika lililofanyika leo Juni 16, 2026 katika Makao ya Taifa Watoto Kikombo.

Kongamano hilo la siku moja, limewakutanisha watoto kutoka katika Kata za Kikombo, Ihumwa na Mtumba likiwa na kaulimbiu inayosema “Mtoto ni Malezi Msingi wa Familia Bora kwa Taifa Imara.” Maadhimisho ya Mtoto wa Afrika ufanyika kila tarehe 16 Juni kila mwaka .