Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Florentino Kyombo, imetembelea na kukagua miradi ya Elimu, Afya na Barabara yenye gharama ya Shilingi bilioni 4,528,354,913 Wilaya Kinondoni.

Ziara hiyo iliyofanyika tarehe 23.06.2026, ililenga kujionea utekelezaji wa miradi ya maendeleo ndani ya Wilaya hiyo ikiwepo Mradi wa Shule ya Sekondari Tarimba Abbas iliyopo Kata ya Tandale, Barabara ya Berege iliyopo kata ya Makumbusho na Mradi wa Kituo cha Afya uliopo Kata ya Mikocheni.

Aidha kamati hiyo imepokelewa na Mheshimiwa Saad Mtambule, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Albert Chalamila akiambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndg Abdul Mhinte, waheshimiwa Madiwani na Menejimenti ya Manispaa ya Kinondoni Pamoja na wataalamu kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam.