Balozi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China, Mheshimiwa Dkt. Suleiman H. Suleiman amewasilisha hati ya uwakilishi kwa Mheshimiwa Bw. Hong Lei, Msaidizi Waziri na Mkugenzi Mkuu wa Idara ya Itifaki ya Serikali ya Jamhuri ya Watu wa Wachina. Shughuli hiyo ikifanyika tarehe 14 Mei 2026 kwenye Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje ya China. Kabla ya hafla hiyo Balozi Suleiman na Bw. Hong Lei walifanya mazungumzo yaliyohusu zaidi kuendeleza ushirikiano wa China na Tanzania katika nyanja mbalimbali ikiwemo masuala ya kijamii, kidiplomasia, Uwekezaji katika Miradi mikubwa ya kimkakati na Uchumi kwa ujumla.