Balozi Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini China, Mheshimiwa Dkt. Suleiman H. Suleiman amewasilisha hati ya uwakilishi kwa Mheshimiwa Bw. Hong Lei, Msaidizi Waziri na Mkugenzi Mkuu wa Idara ya Itifaki ya Serikali ya Jamhuri ya Watu wa Wachina. Shughuli hiyo ikifanyika tarehe 14 Mei 2026 kwenye Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje ya China. Kabla ya hafla hiyo Balozi Suleiman na Bw. Hong Lei walifanya mazungumzo yaliyohusu zaidi kuendeleza ushirikiano wa China na Tanzania katika nyanja mbalimbali ikiwemo masuala ya kijamii, kidiplomasia, Uwekezaji katika Miradi mikubwa ya kimkakati na Uchumi kwa ujumla.
BALOZI SULEIMAN AZUNGUMZA NA NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA CHINA
By John Bukuku
May 14, 2026 | 4:59 pm

Related Stories
View all
Mchanganyiko
5 minutes ago
RAIS DKT. SAMIA AVUNJA BODI YA PSSSF
Mchanganyiko
59 minutes ago
SERIKALI YAWASIHI VIJANA KUEPUKA KUSHIRIKI MIGOGORO YA KIMATAIFA
Serikali imeendelea kuwasihi vijana nchini kujiepusha na ushawishi wa kujiingiza katika migogoro ya kimataifa, ikiwemo vita vinavyoendelea katika baadhi ya mataifa duniani na kusisitiza…