Jaji wa Mahakama Kuu na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Asina Omari akizungumza kwenye mafunzo.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi Hidaya Gwando akielezea lengo la mafunzo.
…………….
Na Hellen Mtereko, Mwanza
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetoa mafunzo kuhusu Sheria,kanuni,maelekezo mchakato na taratibu za uchaguzi kwa waratibu wa uchaguzi wa mikoa,wasimamizi wa uchaguzi,wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi ngazi ya Jimbo,maafisa uchaguzi na maafisa ununuzi 110 kutoka mikoa ya Mwanza na Mara.
Mafunzo hayo ya siku tatu yanafanyika katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Benki Kuu Jijini Mwanza.
Akizungumza kwenye mafunzo hayo Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Uchaguzi, Hidaya Gwando amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uelewa na uwezo wakusimamia shughuli za uchaguzi watendaji wa uchaguzi walioteuliwa ili waweze kuifanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
“Mafunzo haya yanafanyika katika awamu mbili awamu ya kwanza yakifanyika Julai 15 hadi 17 julai 2025 katika vituo saba vya mikoa ya Dodoma,Geita,Iringa,Kagera,Kasikazini unguja,Kigoma,Kilimanjaro,Kusini Unguja,Lindi,mjini Magharibi,Morogoro,Mtwala,Njombe,Ruvuma,Singida,Tabora na Tanga”, Amesema Gwando.
Aidha, kwa sasa Tume ipo katika awamu ya pili ambapo katika awamu hiyo mafunzo yameanza leo Julai 21 na yatamalizika Julai 23 mwaka huu.
“Awamu hii itahusisha Mikoa ya Arusha, Dar es salaam,Kasikazini Pemba,Katavi,Kusini Pemba,Mara,Mbeya,Pwani,Rukwa,Shinyanga,Simiyu,Songwe na Mkoa wa Mwanza”
Awali akifungua mafunzo hayo Jaji wa Mahakama Kuu na Mjumbe wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Asina Omari ametoa maelekezo nane kwa watendaji hao akiwataka kuzingatia maelekezo yatakayotolewa na tume badala ya kufanya kazi kwa mazoea na wazingatie kuwa baadhi ya mambo yamekuwa yakibadilika mathalani kumekuwa na mabadiliko makubwa ya sheria ya uchaguzi wa rais, wabunge na madiwani.
“Vishirikisheni vyama vyote vya siasa vyenye usajili kamili katika hatua zote zenye kuzingatia matakwa ya sheria na katiba ya tume,”amesema Jaji Asina
Jaji huyo pia amewataka kushirikisha wadau wa uchaguzi hususani katika maeneo ambayo kwa mujibu wa Katiba,sheria,kanuni miongozo na maelekezo yatakayotolewa na tume yanatakiwa kushirikishwa huku pia wakitakiwa kufanya utambuzi mapema wa vituo vya kupigia kura na kuhakikisha kunampangilio mzuri na unazozingatia watu wenye ulemavu.
Wanchoke Chinchibera ni msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Ukerewe amesema tofauti na zamani katika awamu hii, majina ya wasimamizi wa majimbo yamechapishwa kwenye mfumo na gazeti la serikali hali itakayoondoa malalamiko yaliyokuwa yanatokea kipindi cha nyuma na hivyo kuufanya uchaguzi kuwa huru na haki.
“Tumeaminiwa na sisi tunaporudi kwenye majimbo yetu tunaenda kutenda haki na kutoleta migogoro miongoni mwa vyama na wadau wa siasa walioko kwenye maeneo yetu kwakuwa sisi tunakuwa sehemu ya utekelezaji wa sheria mpya ya uchaguzi na sio kusababisha migogoro,” amesema Chinchibela.
Kwa upande wake Mohamed Chande, Msimamizi wa uchaguzi wilaya ya Magu amesema baada ya mafunzo hayo wataenda kusimamia haki ya makundi mbalimbali na kukahakikisha kwamba uchaguzi unakuwa huru na waki.