Happy Lazaro,Arusha .
Arusha.Mamia ya Wananchi  wamejitokeza kuiaga miili ya watu 25 waolifariki katika Ajali ya gari iliyotokea mnamo tarehe 24  febuari katika barabara ya Ngaramtoni  namanga Arusha .
Waziri wa Katiba na Sheria Balozi  Dkt Pindi Chana akizungumza  katika uwanja wa mpira Stadium jijini Arusha amesema Mheshimiwa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania samia Suluhu Hassan  alihimiza zoezi hilo liratibiwe na kuhakikisha majeruhi waliopo hospitali wanapata matibabu .
Aidha amesema kama Serikali wataendelea kuwa pamoja na familia hizo kwa ajili ya kuwapumzisha ndugu hao kwani  wameacha pengo  kubwa kwao na kwa serikali.
“ni pigo kubwa kwa  mkoa wa Arusha na kwa Taifa kwa ujumla kwani msiba huu ni wa kwetu sote na hatuna budi kuungana na kuendelea kumwomba Mungu azidi  kutuepusha na majanga mbalimbali “amesema.
Hata hivyo ametaka  vyombo husika kuchukua hatua kali za kisheria kwa wale wote watakaokiuka  sheria za usalama barabarani ili matukio hayo yasiweze kujirudia na kusababisha masafa kama hayo tena.
Naye Mkuu wa mkoa wa Arusha, John Mongela amesema kuwa wameweza kusikiliza maelekezo yote  yaliyotolewa na Rais ambayo  alielekeza  kuhakikisha majeruhi  wote wanapata huduma ikiwemo kuwashika  mkono  ndugu wa waliopoteza maisha katika ajali hiyo. 
Baadhi ya viongozi wa dini na wananchi  walishauri kufanyika ukaguzi wa magari mara kwa mara ili kuepusha ama kusababisha Ajali za mara kwa mara.
Hata hivyo miili hiyo itasafirishwa kwa ajili ya kwenda kupumzishwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Arusha,na wengine  Saba  kutoka mataifa ya nje.