
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi ameongoza kikao kazi kinachohusu mapitio ya Mapendekezo ya Marekebisho ya Sheria ya Jeshi la Polisi na Huduma Saidizi, Sura ya 322,Sheria ya Usalama Barabarani, Sura ya 168,Kanuni za Ada za Usajili wa Shule za Udereva,Kanuni za Usalama Barabarani (Uthibitisho wa Bima za Magari) ya Mwaka 2026,Rasimu ya Mkataba kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Angola kuhusu Masuala ya ulinzi wa raia, Rasimu ya Hati ya Makubaliano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Namibia katika masuala ya urekebu na Rasimu ya Mkataba wa kuhamisha wafungwa kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mauritius.
Kikao hicho kimefanyika Ofisi ndogo ya wizara,jijini Dar es Salaam.
