
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akifuatilia Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2026/2027, kupitia Televisheni ya Taifa (TBC1), Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 11 Juni, 2026. Bajeti hiyo ilikuwa ikisomwa Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar, kwenye Bunge la 13, Mkutano wa tatu katika Kikao cha 48 Jijini Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipiga makofi pamoja na Wasaidizi wake mara baada ya Waziri wa Fedha Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar kumaliza kuwasilisha Hotuba ya Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2026/2027 kwenye Bunge la 13, Mkutano wa tatu katika Kikao cha 48 Jijini Dodoma. Rais Dkt. Samia alikuwa akifuatilia Hotuba ya Bajeti hiyo Kuu ya Serikali kupitia Televisheni ya Taifa (TBC1), Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 11 Juni, 2026.
