Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete akizungumza na Mbunge wa Segerea, Bonnah Kamoli, kabla ya kikao na Wananchi wa Kata ya Kipunguni, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete akizungumza na Mkurgrnzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Mussa Mbura, kabla ya kikao na Wananchi wa Kata ya Kipunguni, jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wananchi wa kata ya Kata ya Kipunguni wakimsikiliza Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete (hayupo pichani) wakati alipozungumza nao jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete akizungumza na wananchi wa kata ya Kipunguni (hawapo pichani) wakati alipokutana nao kutoa msimamo wa Serikali kuhusu fidia na tathmini kwa wakazi hao jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea Bonnah Kamoli. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka wa Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA).
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete akizungumza na Menejimenti ya Mamlaka ya Viwanja vya ndege Tanzania (TAA) wakati wa kikao chake na Menejimenti hiyo na Mbunge wa Segerea, Bonnah Kamoli (mwenye koti la njano, jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete (katikati) akimsikiliza Mbunge wa Segerea, Bonnah Kamoli wakati wa Kikao cha Naibu Waziri huyo na menejimenti ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TAA Mussa Mbura.
Mkurugenzi Mkuu wa TAA Mussa Mbura, akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Atupele Mwakibete (katikati), wakati wakati wa Kikao cha Naibu Waziri huyo, Mbunge wa Segerea Bonnah Kamoli (kulia) na Menejimenti ya TAA kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
PICHA NA WUU
………………………………………
Serikali imewahakikishia Wakazi wa Kata ya Kipunguni, jijini Dar es Salaam kuwa itaanza zoezi la tathmini kwa wakazi wote wa maeneo hayo ndani ya wiki moja ijayo ili kupisha upanuzi wa kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Akizungumza katika Mkutano wa hadhara jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Atupele Mwakibete, amefafanua kuwa zoezi hilo litasaidia wakazi hao kufahamu kiasi ambacho Serikali itawalipa.
“Niwahakikishie kuwa pamoja na muda mrefu mliosubiri Serikali Sikivu ya Mama Samia inatekeleza yale yote inayoahidi na sasa inaanza na zoezi la tathmini na baada ya hapo zoezi la malipo litafuata”, amesisitiza Naibu Waziri Mwakibete.
Naibu Waziri Mwakibete amewataka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) pamoja na Taasisi zinazohusika kuhakikisha inatoa elimu kabla ya zoezi la tathmini ili kupunguza malalamiko mara baada ya zoezi la tathmini kukamilika.
Naye Mbunge wa Segerea, Bona Kamoli, ameishukuru Serikali kwa kutimiza ahadi na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano wakati wa zoezi hilo ili likamilike kwa wakati.
Aidha, Bona ameisisitiza TAA kuhakikisha wanapitia nyumba zote ili kujua wahusika halisi kwa lengo la kuepuka changamoto za udanganyifu wakati wa malipo ya waathirika.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Mussa Mbura, ametoa wito kwa wananchi kuanza kuwa na taarifa zote muhimu ili kurahisisha la tathmini na kulifanya kuwa taarifa muhimu.
“Niwasihi wananchi wa kata ya Kipawa kwakuwa zoezi hili ni la muhimu na linahusisha watu wengi ni muhimu kuwa na taarifa muhimu ili kupunguza muda wa kulikamilisha’ amesisitiza Mussa.
Zoezi la tathmini ambalo litahusisha uhakiki, tathmini na uthamini wananchi wa Kipunguni jijini Dar es Salaam linatarajiwa kufanywa kwa zaidi ya watu 1100.