WENYEJI, Wydad Athletics wamefanikiwa kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya ushindi wa 2-0 dhidi ya waliokuwa mabingwa watetezi, Al Ahly ya Misri usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Mfalme Mohamed V Jijini Casablanca nchini Morocco.
Mabao yote ya Wydad yamefungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Morocco, Zouheir El-Moutaraji mwenye umri wa miaka 26, moja kila kipindi, la kwanza dakika ya 15 na la pili dakika ya 45.
WYDAD CASABLANCA MABINGWA AFRIKA 2022
