Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Joelson Mpina kwa Mamlaka aliyopewa chini ya Sheria ya Maziwa Namba 8 ya Mwaka 2004 ametengua uteuzi wa Kaimu Msajili wa Bodi ya Maziwa, Dkt. Sophia Mlote, kufuatia kutoridhishwa na utendaji wake wa kazi. Uteuzi wa Msajili wa Bodi ya Maziwa utafanyika baadae.