Robert Lewandowski akishangilia baada ya kuifungia Bayern Munich mabao mawili dakika za 34 na 62 katika ushindi wa 3-2 dhidi ya wenyeji, Olympiacos kwenye mchezo wa Kundi B Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa Georgios Karaiskáki mjini Piraeus. Bao lingine la Bayern Munich lilifungwa na Corentin Tolisso dakika ya 75, wakati ya Olympiacos yalifungwa na Youssef El-Arabi dakika ya 23 na Guilherme dakika ya 79 na kwa mabao yake mawili jana, Lewandowski amepanda nafasi ya tano katika orodha ya wafungaji bora wa muda wote wa Ligi ya Mabingwa Ulaya PICHA ZAIDI SOMA HAPA
LEWANDOWSKI AIPA USHINDI BAYERN MUNICH UGENINI LIGI YA MABINGWA ULAYA
By Alex Sonna
October 23, 2019 | 4:17 am

Related Stories
View all
Michezo
44 minutes ago
UJERUMANI YAIFUMUA CURACAO KWA KIPIGO CHA 7-1 KOMBE LA DUNIA
Timu ya Taifa ya Ujerumani imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 7-1 dhidi ya Curacao katika mchezo wa hatua ya makundi ya Kombe la…
Michezo
4 hours ago
SIMBA SC YAENDELEZA MAKALI YAKE, YAICHAPA PAMBA JIJI 2-1
Wekundu wa Msimbazi, Simba SC, wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Pamba Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Mabao…
