RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Watendaji wa SMZ Kisiwani Pemba katika ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi Pemba, kushoto Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Issa Haji Gavu na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na kulia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa na Idara Maalum za SMZ.Mhe.Haji Omar Kheri.mkutano huo umefanyika leo wakati wa ziara yake Kisiwani PembaRAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Watendaji wa SMZ Kisiwani Pemba wakati wa ziara yake, mkutano huo umefanyika katika ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi Pemba, kushoto Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.Mhe.Issa Haji Gavu, Mke wa Rais wa Zanzibar.Mama Mwanamwema Shein na Mshauri wa Rais Pemba.Mhe. Maua Abeid Daftari.WAZIRI wa Nchi Ofisa ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Issa Haji Gavu, akizungumza na Watendaji wa Wizara za SMZ Kisiwani Pemba kabla ya kumkaribisha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.Mhe.Dk.Ali Mohamed Shein, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta ya Makonyo Wawi Pemba.(Picha na Ikulu)
…………………….
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameeleza kuwa Maafisa Wadhamini wanadhima kubwa ya kuwasimamia wale wote wanaovunja misingi ya kukuza uchumi hapa nchini.
Dk. Shein aliyasema hayo leo, huko katika ukumbi wa Kiwanda cha Mafuta na Makonyo Wawi wakati alipokutana na Watendaji na Viongozi Wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar pamoja na viongozi wa vikosi vya SMZ na SMT wanaofanya kazi zao kisiwani Pemba.
Rais Dk. Shein alieleza kuwa, kwa mwaka jana kasi ya ukuaji wa uchumi wa Zanzibar ilifikia asilimia 7.1 na matarajio ni kukua kwa uchumi huo mwaka hadi mwaka kutokana na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.
Alisema kuwa mapato yanakusanywa kwa ufanisi mzuri na kinachokusanywa ndicho kinachotumika na hakuna tatizo la matumizi ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa hivi sasa.