Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti (kushoto) akimkaribisha Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike ofisini kwake baada ya Kamishna Jenerali Kasike kufanya ziara katika Wilaya ya Bukoba na kwenda kumsalimia ofisini kwake.
Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akiweka saini katika kitabu cha wageni alipokaribishwa katika ofisi ya Mkuu wa Magereza mkoa wa Kagera.
Mkuu wa gereza la kilimo la Rwamulumba, Mrakibu Msaidizi Elly M Jacob akimkaribisha Kamishna Jenerali Phaustine Kasike kuingia ndani ya gerezani ili kufanya ukaguzi.
Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akitoa maelekezo kwa Koplo Arnold ambaye ni mganga wa gereza la kilimo la Rwamulumba.
Mkuu wa gereza la kilimo la Rwamulumba, Mrakibu Msaidizi Elly M Jacob akimpa ufafanuzi Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike kuhusu kilimo cha chai na changamoto zake alipomtembeza Kamishna Jenerali Kasike kwenye shamba hilo la chai lililopo katika gereza la kilimo la Rwamulumba.
Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike akizungumza na wafungwa pamoja na Mahabusu wa gereza kuu la Bukoba .
Baadhi ya Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza kutoka Magereza Mkoa wa Kagera, Gereza Bukoba na Gereza Rwamulumba, wakimsikiliza Kamishna Jenerali wa Magereza Phaustine Kasike(hayupo pichani) alipofanya kikao nao kwenye ukumbi wa gereza Bukoba.
Mamalaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeahidi kuendeleza mashirkiano na Mamlaka ya Mafunzo ya Amali Zanzibar katika kutoa elimu na mafunzo…
******* Taka zinazozalishwa katika masoko zimeelezwa kuwa zinaweza kubadilishwa kuwa bidhaa zenye thamani na kuwa chanzo cha kipato. Mwanzilishi na Mwenyekiti wa GEHESE, Liliani…