************************************

Makamo wa kwanza wa Rais wa SMZ Maalim  Seif Sharif Hamad amesema amejidhatiti kumshauri na kutimiza majukumu yake atakayopangia na Rais wa Zanzibar Dk Hussein Ali Mwinyi kwa kwa mujibu  wa Katiba.
Amesemai ameridhishwa na malengo ya  utendaji wa kazi za serikali za  kuondosha kadhia za rushwa, ubadhirifu na ukwapuzi  wa mali za umma.
Msimamo huo umetolewa na Makamo huyo wa kwanza wa Rais zanzibar Maalim  Seif  Sharif Hamad aliyesema atatimiza  wajibu  wake wa kumshauri Rais ili kushamirisha maendeleo .
Amesema  kwakuwa yeye ni makamp wa kwanza Rais  SMZ atatekeleza majukumu hayo na mengine atakayopangiwa na Rais .
Amesema hatakaa kimya atakapopoona mambo yakienda  shaghalabaghala  au kuyatazama bila kuichukua hatua  kwa niaba ya Serikali.
Aidha Mwanasiasa huyo mkongwe  amesema kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa(SUK) si matakwa ya kisiasa bali ni mahitaji ya kikatiba na kisheria  .
Amesema   kuwepo kwa serikali hiyo ni maamuzi yaliotokana na rodhaa pia utashi wa wananchi  wote wa zanzibar.
Maalim seif amesema  serikali haitamvumilia watendaji wavivu, wazembe na wapiga porojo au wenye urasimu badala yake kila mmoja atimize wajibu  wake.
Amesema hayo ni  matakwa ya Rais yanayomtaka kila mtendaji  smz kujituma bila kusimamiwa kwani Rais anavhotaka no uadilfu na uwajibikaji katika uendeshaji wa seriakli yake.
Maalim seif amesema kinachotakiwa ni kulauniwa kiwango cha ufanisi , nidhamu kwa kufuata  sheria na motisha utakaoongeza  tija na  kuleta manufaa.