Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Diwani wa Kata ya Ngarenaro jijini Arusha, Mheshimiwa Abdulaziz Abubakar Chende, maarufu kwa jina la kisanii Janjaro (zamani Dogo Janja), akimwonesha Rais picha aliyopiga naye Ikulu Dar es salaam mwaka 2010, walipokutana jijini Arusha jana. 

Rais Mstaafu alikuwa mkoani humo kushiriki Mkutano wa Kamati ya Tuzo za Chakula Barani Afrika (Africa Food Prize Committee – AFP), uliofanyika Julai 23–24, 2026. Dkt. Kikwete ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo inayofanya kazi chini ya Jukwaa la Mabadiliko ya Kijani Barani Afrika (AGRA), ambalo hutambua na kutoa tuzo kwa taasisi na watu binafsi waliotoa mchango mkubwa katika kuendeleza sekta ya kilimo na usalama wa chakula barani Afrika.