Afisa Uhusiano Kampuni ya ETDCO Bi. Samia Chande (wa pili kulia) akitoa elimu leo Julai 9, 2026 kwa wananchi waliotembelea banda la Kampuni hiyo katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba)

………….

Kampuni ya ETDCO leo, Julai 9, 2026, imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme kupitia banda lake katika Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.