Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Ijumaa (Julai 3, 2026), ametembelea na kuweka shada la maua katika Kaburi la Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, lililopo Butiama, mkoani Mara.

Dkt. Mwigulu yuko mkoani Mara kwa ziara ya kikazi ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi.