Ujenzi wa Mtambo wa Kisasa wa Kuchakata Maji Taka wa Mbezi Beach jijini Dar es Salaam
Utekelezaji wake umefika asilimia 70 ambapo mradi ukikamilika katika awamu ya kwanza utakuwa na uwezo wa kuchakata maji taka yenye ujazo wa mita za ujazo 16,000 kwa siku kwa kuhudumia maeneo ya Mbezi Beach na Kawe.
Mradi utaongezewa uwezo wa kuchakata maji taka hadi kufikia mita za ujazo elfu 22 kwa siku ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya huduma za usafi wa mazingira katika maeneo hayo.

