Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ,akizungumza  wakati akifungua Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Afya ya Msingi nchini Tanzania ulioambatana na uzinduzi wa   namba 115 ya kuwasiliana na watoa huduma kupitia mfumo wa M-mama ulioanza leo Machi 25,2024 jijini Dodoma.

Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko  wakati akifungua Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Afya ya Msingi nchini Tanzania ulioambatana na uzinduzi wa   namba 115 ya kuwasiliana na watoa huduma kupitia mfumo wa M-mama ulioanza leo Machi 25,2024 jijini Dodoma.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI anaeshughulikia Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Mhe.Dkt. Festo Dugange ,akizungumza  wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Afya ya Msingi nchini Tanzania ulioambatana na uzinduzi wa   namba 115 ya kuwasiliana na watoa huduma kupitia mfumo wa M-mama ulioanza leo Machi 25,2024 jijini Dodoma.

Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Godwin Mollel,akizungumza  wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Afya ya Msingi nchini Tanzania ulioambatana na uzinduzi wa   namba 115 ya kuwasiliana na watoa huduma kupitia mfumo wa M-mama ulioanza leo Machi 25,2024 jijini Dodoma..

 

NAIBU  Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, akizindua  namba 115 ya kuwasiliana na watoa huduma kupitia mfumo wa M-mama unaoratibiwa katika hospitali za mikoa kupitia waratibu waliopewa mafunzo.

NAIBU  Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua  Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Afya ya Msingi nchini Tanzania ulioambatana  na uzinduzi wa namba namba 115 ya kuwasiliana na watoa huduma kupitia mfumo wa M-mama  leo Machi 25,2024 jijini Dodoma

 

NAIBU  Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko,akipongeza zawadi kutoka kwa Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI anaeshughulikia Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Mhe. Festo Dugange,iliyotolewa kwa ajili ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutambua na kuthmani mchango wake katika kuimarisha huduma za Afya ya Msingi.

Mkurugenzi wa M-Mama  Tanzania Bi.Dolorosa Duncan ,akizungumza na waandishi wa habari  wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Afya ya Msingi nchini Tanzania ulioambatana na uzinduzi wa   namba 115 ya kuwasiliana na watoa huduma kupitia mfumo wa M-mama ulioanza leo Machi 25,2024 jijini Dodoma.

 

Na.Alex Sonna-DODOMA

NAIBU  Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko,ameupongeza  mfumo wa usafiri wa dharura kwa wajawazito, waliojifungua na watoto wachanga (M-MAMA)uliobuniwa na Watanzania .

Dkt. Biteko ametoa pongezi hizo wakati akifungua  Mkutano wa Kwanza wa Kimataifa wa Afya ya Msingi nchini Tanzania ulioambatana  na uzinduzi wa namba namba 115 ya kuwasiliana na watoa huduma kupitia mfumo wa M-mama unaoratibiwa katika hospitali za mikoa kupitia waratibu waliopewa mafunzo kwa ambapo kila mkoa wanaweza kutoa huduma hizo ulioanza leo Machi 25,2024 jijini Dodoma

Amesema kuwa kila mwaka  akina Mama zaidi ya milioni mbili, laki tatu na sabini wanajifungua, na kati ya hao takriban akinamama elfu arobaini na tano wanapata dharura zinazohitaji usafiri kwenda kwenye kituo kinachotoa huduma stahiki kulingana na dharura hizo.

“Kwa furaha kubwa nasimama mbele yenu siku ya leo nikifurahia kuona maono ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha mfumo wa usafiri wa dharura kwa wajawazito, waliojifungua na watoto,” amesema Dkt. Biteko.

Dkt.Biteko amesema, M-mama inaratibiwa katika hospitali za mikoa kupitia waratibu waliopewa mafunzo kwa kupiga namba 115 ambapo waratibu wa m-mama katika kila mkoa wanaweza kutoa huduma hizo.

“Napenda kuwashukuru wadau wetu wa maendeleo Vodacom Tanzania, Vodafone Foundation, USAID, Benki ya Dunia na wadau watekelezaji wa mfumo wa ‘Touch Health’ na ‘Pathfinder International’ kwa mchango wao katika kushirikiana na Serikali kuleta huduma hii inayohitajika kwa wote,” amesisitiza Dkt. Biteko.

Hata hivyo Dkt. Biteko ameagiza kuweka Mpango Mkakati wa kuhakikisha uwekezaji wa miundombinu uliofanywa na Serikali katika vituo ngazi ya Afya ya Msingi inatunzwa.

Dkt. Biteko amewataka kujadili kwa kina namna bora ya kubuni mbinu zitakazowezesha kuongeza kasi ya kuajiri wataalam wa kada mbalimbali za afya hasa zile zenye upungufu mkubwa.

“Naagiza kuainisha mikakati ya utoaji wa elimu ya afya kwa jamii ili wananchi waelimishwe kuhusu njia za kuzuia magonjwa, umuhimu wa chanjo na njia zingine za kudumisha afya bora.”amesema

Dkt. Biteko amehimiza kuwezesha watu, familia na jamii kwa ujumla kuzingatia afya bora na kuhamasisha utekelezaji wa sera na miongozo inayolenga kulinda afya ya jamii.

Pia Dkt. Biteko amesisitiza kuimarisha mifumo ya ufuatiliaji na tathmini ya huduma za afya ya msingi ili kuweza kufahamu maendeleo ya utekelezaji wa Afua mbalimbali za afya na kutambua maeneo ya kuboresha.

Awali Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI anaeshughulikia Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe, Mhe. Festo Dugange amesema  kuwa mkutano huo unawezesha kujadiliana masuala mbalimbali na kubadilishana uzoefu na namna ya kuboresha afya ya msingi kwa watu wote.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Afya, Mhe. Godwin Mollel amewashukuru wafanyakazi wa afya nchini kwa kujitolea kuboresha huduma za afya ambapo kupitia wao idadi ya vifo vya akinamama wajawazito vimepungua kutoka 556 hadi 104 mwaka 2023.

Hata hivyo, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya kuboresha sekta ya afya ambapo shilingi trilioni 6.7 zilitolewa ili kuimarisha miundombinu, dawa, vifaa na tiba pamoja na kuongeza rasilimali watu ambao ndiyo nguvu muhimu za kufikisha huduma bora kwa wananchi.
Naye Mkurugenzi wa udhibiti Vodacom Tanzania Bw.Agapinus Tax, amesema kuwa kampuni hiyo inaunga mkono Mfumo wa Usafirishaji wa Dharura kwa Wajawazito na Watoto Wachanga (M-MAMA).
“Ushiriki wetu unaonesha azma yetu ya kutumia teknolojia kutatua changamoto za afya hasa katika huduma za uzazi na watoto wachanga,”amesema.
Amesema Mwaka 2022 katika uzinduzi wa mfumo huo Rais Samia Suluhu Hassan alielekeza kushirikiana na serikali ili umfikie kila mwananchi na waliitika wito na sasa umesambaa nchi nzima.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa M-Mama  Tanzania Bi.Dolorosa Duncan amesema kuwa namba ya huduma ya dharura ya 115 ni kwa ajili ya kina mama  wajawazito na waliojifungua Chini ya siku 42 na watoto wachanga wenye dharura na sio wamama waliopatwa na uchungu wa kujifungua.
“Kwa sasa huduma hii ya Simu ya dharura inatolewa kwa ngazi kituo kimoja cha afya na kingine nchi nzima ila kwa mkoa wa Shinyanga huduma hii ya dharura imefikia mpaka ngazi ya Jamii na sasa tunaongeza  Mikoa mitano ya Tanzania Bara na Mkoa mmoja wa Tanzania Visiwani na malengo yetu ni kufika katika mikoa yote Tanzania,” ameeleza Dolorosa
Pia ameishukuru serikali Kwa kuendelea kutoa Ushirikiano kwa Sekta binafsi na kuahidi kuendelea kufanya kazi ili kuhakikisha mfumo huu unamfikia mpaka mama mjamzito akiwa nyumbani na akipata dharura yeyote basi aweze kupiga 115 na kupata huduma bila kikwazo chochote.