Mkaguzi Mkuu wa ndani wa serikali ,Athumani Selemani Mbuttuka akizungumza katika mahafali  hayo jijini Arusha leo. 
Baadhi ya wahitimu katika chuo cha uhasibu Arusha wakiwa katika mahafali yao jijini Arusha leo.
********************
Julieth Laizer,Arusha.
Arusha.Mkaguzi Mkuu wa ndani  wa serikali,Athumani Selemani Mbuttuka ametoa wito  kwa vyuo  nchini kufanya mabadiliko ya  mitaala yao ili kuwezesha ufundishaji kwa vitendo  ili kuendana na mahitaji ya soko .
Ameyasema hayo leo jijini Arusha  wakati akimwakilisha Waziri wa fedha,Dk Mwigulu Nchemba  katika mahafali ya 24 ya wanafunzi wa chuo cha uhasibu Arusha (IAA) ambapo jumla ya wanafunzi 3,529 wamehitimu kozi mbalimbali.
Amesema kuwa,mafunzo kwa vitendo bado hayapewa umuhimu katika vyuo mbalimbali ,hivyo ni wajibu wao kuhakikisha wanafanya mabadiliko ili kuondokana na changamoto  ya ajira  .
“Tunaomba pia vyuo vyetu  wahakikishe wanajikita kwenye maswala ya tabia  ya nchi katika kuhakikisha kunakuwepo na mitaala vyuoni ili wanafunzi waweze kufahamu wakiwa vyuoni, huku akivitaka  vyuo kujikita katika kufanya taifiti kwenye rasilimali na uimarishaji wa fedha”amesema .
Kwa upande wake Kaimu  Mkuu wa chuo cha uhasibu  Arusha ,  Dk .Cairo Mwaitete 
amesema kuwa,chuo hicho kimepiga hatua kubwa kwa kuwa na wanafunzi wengi  kutoka wanafunzi 3,000 mwaka 2017/18 hadi wanafunzi 13,000 kwa mwaka huu wa fedha ,na  kimekuwa kikifanya tafiti mbalimbali ambazo zina lengo  la kutoa elimu bora itakayosaidia kutatua changamoto katika jamii.
Mwaitete amesema kuwa,chuo hicho kimejiwekea mikakati ya kuongeza mitaala mingine katika ngazi ya astashahada  na shahada  kwa lengo la kuwafikia  wengi zaidi na kwenda kutatua changamoto  katika jamii.
“Tumeona kuna haja ya kujipanua zaidi na hivyo tunaangalia namna ya kushirikiana na jeshi la polisi katika kutoa elimu juu ya matumizi ya kompyuta  na  vifaa ili kuweza kuwaandaa walinzi wa mitandaoni watakaolinda fedha zetu kwenye mabenki.”amesema Mwaitete.
Ameongeza kuwa ,wanataka kuhakikisha wanaendelea kusaidiana na serikali katika kuandaa mafunzo ya usalama na taarifa na kujiepusha na makosa mbalimbali yanayotokea  mitandaoni. 
Amefafanua kuwa, chuo hicho kimekuwa kikiunga mkono sera ya serikali ya kupeleka elimu katika maeneo ya pembezoni  huku wakihahakisha wanaboresha mitaala ili iweze kuendana na wakati   na kuwezesha wanafunzi
Aidha amewataka wahitimu hao kuweza kujiajiri wao wenyewe huku wakizitafuta  fursa mbalimbali  ambazo zipo katika nchi yetu  ambazo zikitumiwa vizuri zitaweza  zitaweza  kutatua  changamoto  ya ajira. 
 Naye  Mwenyekiti wa bodi ya chuo hicho,Dk Mwamini Tulli amesema 
kuwa,katika mahafali ya mwaka 2021 walikuwa jumla ya wahitimu 2,481 ambao walitunukiwa  vyeti  katika ngazi nne tofauti ambazo ni shahada za uzamili,shahada,stashahada na astashahada ambapo aliwataka wahitimu hao kutumia  elimu yao kupambana na maisha na wasitegemee  ajira  bali  wajiamini kuwa  wanaweza ili wasiendelee  kutembea na vyeti. 
Mkuu wa wilaya  ya Ngorongoro ambaye ni mmoja wa wahitimu, Raymond Mangwala  amesema kuwa,ameweza kupata uelewa mkubwa  juu ya matumizi ya Tehama kwa viongozi  hususani katika usimamizi wa miradi ya maendeleo,utatuzi wa migogoro,uandaaji wa  biashara ,ambapo  itawezesha miradi hiyo kufanyika kwa weledi na uaminifu mkubwa .