Mkurugenzi wa  shule ya mchepuo wa  kiingireza ya Tumaini Senior iliyopo Monduli,Modest Bayo  akizungumzia kuhusiana na programu  hizo wanazotoa shuleni  hapo  kwa lengo ya kuwawezesha wanafunzi kujiajiri pindi wanapohitimu masomo yao.
Mwenyekiti wa  chama cha walimu mkoa wa  Arusha, Lotha  Laizer akizungumza katika hafla hiyo ya wanafunzi wa  shule ya Tumaini Senior kuonyesha bunifu zao wanazofanya shuleni hapo. 
Wanafunzi wa  shule ya sekondari ya  mchepuo  wa  kiingireza ya Tumaini  Senior iliyopo wilayani Monduli mkoani Arusha wakionyesha moja  ya programu wanayofanya ya mafunzo kwa vitendo kuhusu maswala la DNA .
……………………………..
Julieth Laizer ,Arusha
Zaidi ya  wanafunzi 200  wameweza kunufaika na programu  ya elimu kwa vitendo  (PBL) ambayo inawaandaa kuweza  kujiajiri na kuondokana na changamoto  za ajira pindi wanapohitimu kidato cha nne na cha sita. 
Aidha programu hiyo ambayo inatolewa na shule ya mchepuo wa  kiingireza ya sekondari Tumaini Senior iliyopo wilayani Monduli mkoani Arusha imeweza kuwanufaisha wanafunzi hao  ambapo asilimia kubwa wameweza kuwa wabunifu kwa kutengeneza vitu mbalimbali  kulingana na elimu waliyoipata.
Akizungumzia kuhusiana na programu hiyo katika hafla ya kuonyesha  bunifu hizo  ,Mkurugenzi wa  shule hiyo, Modest Bayo amesema kuwa programu hiyo ilianzishwa shuleni hapo tangu mwaka 2016 ambapo programu  hufanyika  nje ya masomo  ya darasani huku wanafunzi wakipata  muda  wa kujifunza kwa vitendo kulingana na uhitaji  wao  .
“Programu hiyo kwa njia ya vitendo imegawanyika katika ngazi  mbalimbali ikiwemo utafiti kwa ajili ya malaria ,uandishi wa habari,na utafiti juu ya vinasaba (DNA) ambapo vyote hivyo tunafanya kwa vitendo huku  kila mwanafunzi akionyesha jinsi alivyojifunza.”amesema. 
Ameongeza kuwa, tangu kuanza kwa programu  hiyo imeweza  kuwajengea  wanafunzi upeo mkubwa na uelewa  katika uhalisia wa darasani ambapo kupitia programu hiyo imewasaidia wanafunzi wengi waliohitimu  kuweza kujiajiri pindi wanapohitimu masomo yao huku nakusubiri kuendelea na masomo  jambo ambalo linawafanya kuweza kuwa wabunifu na kuweza  kuisaidia  jamii  inayowazunguka .
Naye Mwalimu mkuu wa  shule hiyo,Sifael Martin  amesema kuwa mbali na utafiti hizo pia wameweza kufanya  utafiti katika maswala ya Google kwa kutumia  kompyuta  huku  wakitengeneza Robot inaweza  kuruka  juu ikiendeshwa  kwa njia ya programu ya drons. 
Amesema kuwa, mbali na programu  hiyo ya PDL wamekuwa wakitoa  programu ya Stemm ambayo inamwezesha  mwanafunzi kufundishwa maswala  ya Kompyuta  Science  ambayo hujifunza lugha  ya kompyuta  katika kutengeneza  programu  ikiwemo website.
Kwa upande wake ,Mwenyekiti wa chama cha walimu mkoa wa Arusha,  Lotha Laizer amesema kuwa, uwepo kwa programu  hiyo  mashuleni ni muhimu sana kwa wanafunzi kwani inawawezesha kuweza kujiajiri pindi wanapomaliza  kwani anakuwa na ubunifu wake  tayari  ambao  unamwezesha  kujiajiri katika  sekta mbalimbali.
Aidha ameomba serikali kuanzisha  programu  hiyo katika shule za serikali ili kuweza  kuwaandaa  wanafunzi kuweza kujiajiri  na kuondokana na changamoto  ya ajira  ambayo imekuwa ni  changamoto  kubwa kwa wahitimu  wengi na kuweza kujiajiri na kuwa wanasayansi  wazuri wa kusaidia wengine. 
Mmoja wa wanafunzi shuleni hapo,Given Malyango kidato cha nne anayefanya programu ya utafiti wa  panya na vyura wanavyoweza kutumika kwa ajili ya kujifunzia  kwa vitendo alisema kuwa, walianza kwa kufuga  panya wawili ambao wanatumika kufanyia utafiti shuleni hapo ambapo wameweza kuwafuga  wakazaliana na kuweza  hukupatikana panya  kumi na moja  kwa sasa ambao wanatumika  kwa ajili ya kufanyia  utafiti  shuleni hapo.