Mamalaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imeahidi kuendeleza mashirkiano na Mamlaka ya Mafunzo ya Amali Zanzibar katika kutoa elimu na mafunzo ya ufundi stadi yenye ubora kwa kwa wananchi wa pande zote mbili za Tanzania bara na Zanzibar.Mkurugenzi Mkuu wa VETA CPA Anthony Kasore amesema hayo  14 Agasti, 2026 alipotembelea mabanda ya VETA na VTA katika Tamasha la Kizimkazi lililokuwa likifanyika katika viwanja vya Dimbani Kusini Unguja, Zanzibar.

“niwashukuru wenzetu wa VTA kwa kuendelea kushirikiana nasi na tutahakikisha ushirikiano wetu unadumu na unazidi kuimarika siku hadi siku ili kuhakikisha wananchi wa visiwani na bara wanapata mafunzo ya ufundi stadi yenye ubora na yanayowawezesha kushiriki kikamilifu kwenye shuguli za kiuchumi na kijamii,” Amesema CPA Kasore.

CPA Kasore ameongeza kwa kusema, “tunamshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutembelea banda letu kipindi cha tamasha hili, lakini pia tunashukuru kwa nguvu kubwa aliyoiweka katika upanauzi wa vyuo, tunawashukuru pia viongozi wengine wote waliopita na kututembelea na kutoa ushauri na maoni yao tumeyapokea na tutayafanyia kazi.”

Sambamba na hilo CPA Kasore amesema VETA imepokea maoni na mapendekezo kutoka kwa wahitimu wa VETA kuhusu kuongezwa kwa vyuo vinavyotoa mafunzo ya matengezo ya simu za mkononi pamoja na kuongeza muda wa kutoa mafunzo hayo kuwa mrefu na si muda mfupi pekee kama ilivyo sasa.

CPA  Kasore amehitimisha kwa kuishukuru Tasisi ya Mwanamke Initiative kwa kuipa VETA mwaliko wa kushiriki katika Tamasha hilo kwa kushirikina na VTA kwani imeleta manufaa makubwa kwa wananchi wa visiwani ambao wamepata taarifa za kutosha kuhusu mafunzo ya ufundi stadi lakini pia huduma zitoleazo na vyuo vya VETA.