Mwenyekiti wa NMB Business Club Mkoa wa Dar es Salaam na Mjumbe wa Bodi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Awadhi Mpandila, akizungumza wakati wa semina ya NMB Business Club iliyofanyika Dar es Salaam. Walioketi meza kuu ni Reynold Tony Lusingu, Meneja Mwandamizi wa Idara ya Biashara Benki ya NMB; William Nkuna, Kaimu Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam; Petro Kyando, Katibu wa NMB Business Club; na Leah Mwakang’ata, Mkuu wa Idara ya Amana za Biashara (kulia) wa Benki ya NMB.
Mkuu wa Idara ya Amana za Biashara Benki ya NMB, Leah Mwakang’ata, akizungumza wakati wa semina ya NMB Business Club iliyofanyika Dar es Salaam. Walioketi meza kuu ni Reynold Tony, Meneja Mwandamizi wa Idara ya Biashara Benki ya NMB; William Nkuna, Kaimu Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam; Awadhi Mpandila, Mwenyekiti wa NMB Business Club Mkoa wa Dar es Salaam; na Petro Kyando, Katibu wa NMB Business Club.
………………
Benki ya NMB imeendelea kuimarisha huduma kwa wafanyabiashara kupitia NMB Business Club, jukwaa linalowapa wateja elimu ya fedha, teknolojia na fursa mbalimbali za kukuza biashara zao kwa uendelevu. Semina hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Cardinal Rugambwa, Dar es Salaam.
Akizungumza katika semina hiyo, Mwenyekiti wa NMB Business Club Mkoa wa Dar es Salaam na Mjumbe wa Bodi ya Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania (JWT), Award Mpandila, alisema jukwaa hilo limekuwa muhimu kwa kuwaunganisha wafanyabiashara na kuwajengea uwezo wa kutumia mifumo rasmi ya kifedha. Aliwahimiza wafanyabiashara kupitisha mauzo yao kupitia benki ili kujenga historia nzuri ya kifedha inayoweza kuwasaidia kupata huduma mbalimbali, ikiwemo mikopo.
Kwa upande wake, Meneja Mwandamizi wa Business Banking Benki ya NMB, Reynold Tony, alisema benki hiyo itaendelea kutoa bidhaa, elimu na suluhisho zinazolenga kuimarisha biashara za wateja wake. Alisema NMB inalenga kuwa mshirika wa karibu wa wafanyabiashara katika kujenga biashara imara na zinazoweza kukabiliana na mabadiliko ya soko.
Baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria, akiwemo Eileen Kunaga na Ally Kuburi kutoka Ilala, walisema jukwaa hilo limewasaidia kupata elimu kuhusu matumizi ya sola, usimamizi wa fedha na huduma za taasisi mbalimbali, ikiwemo TRA. Walisema maarifa hayo yanaweza kupunguza gharama za uendeshaji na kusaidia biashara kukua kwa muda mrefu.

