Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, leo tarehe 20 Mei 2026 amewasili mkoani Arusha kwa shughuli za Kikazi. Pamoja na mambo mengine Mhe. Makamu wa Rais anatarajiwa mgeni rasmi katika Mkutano wa 13 wa Kitaaluma wa Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA) utakaofanyika kesho tarehe 21 Mei 2026 katika Ukumbi wa Ngurudoto mkoani Arusha.