‎Na Meleka Kulwa-Fullshangwe Blog, Bungeni Dodoma

‎Serikali imeendelea kuajiri wataalamu mbalimbali katika Sekta ya Afya ambapo jumla ya wataalamu 53,633 wameajiriwa kuanzia mwaka 2021 hadi Machi 2026.

‎Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema kuwa wataalamu hao wamesambazwa katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini ili kuimarisha utoaji wa huduma.

‎Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo , Mei 11, 2026, bungeni jijini Dodoma, Waziri wa Afya, Mhe. Mohamed Mchengerwa amebainisha kuwa watumishi 9,039 wameajiriwa kwa mikataba ya muda mfupi kupitia mapato ya ndani ya vituo vya afya.

‎Pia ameongeza kuwa Serikali imeanzisha Programu ya Samia Health Super Specialization Scholarship kwa ajili ya kuongeza wataalamu bingwa na bingwa bobezi.

‎Amesema kuwa wataalamu 2,982 wamepata mafunzo ya ubingwa na ubingwa bobezi kuanzia mwaka 2021/2022 hadi Machi 2026.

‎Aidha amesema kuwa hatua hiyo imeongeza uwezo wa utoaji wa huduma za ubingwa nchini na kupunguza utegemezi wa matibabu nje ya nchi.