Mkufunzi Dkt .Kassim Hussein Kassim akiwasilisha mada katika Mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji wa mfuko wa huduma za Afya huko Ukumbi wa ZSSF Michenzani mall mjini Unguja.

Baadhi ya wajumbe wa mfuko wa huduma za Afya ZHSF wakiwa katika mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji wa mfuko huo huko Ukumbi wa ZSSF Michenzani mall mjini Unguja.

PICHA NA FAUZIA MUSSA -MAELEZO ZANZIBAR

Na Rahma Khamis Maelezo.

Mwenyekiti wa Bodi wa Mfuko wa Huduma za Afya  Zanzibar  (ZSHF) Mbarouk Omar Muhammed amewataka watendaji wa Mfuko huo kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yaliyokusudiwa. 

Ameyasema hayo huko Ofisi za Mfuko huo Michenzani Mall wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji na Uongozi wa Mfuko huo.

Amesema kuwa Mfuko huo ni wa kila  mwananchi hivyo ipo haja kwa watendaji hao  kuongeza bidii zaidi katika utendaji  ili kutoa huduma bora na za  uhakikakwa wote .

Aidha amefahamisha kuwa  lengo la mafunzo hayo  ni kuendeleza huduma za afya ili wananchi wote waweze kupata matibabu kwa  gharama nafuu.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yatawasaidia watendaji kupanga mikakati madhubuti itakayopelekea kufanya kazi zao kwa ufanisi ili kuendeleza Mfuko huo na kutoa huduma bora kwa wote.

 Mapema kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ZSHF Yassin Ameir Juma amesema Mfuko huo bado ni mpya hivyo mafunzo hayo yatasaidia katika utendaji mzuri  ili kila mwananchi kupata huduma za afya.

Aidha amewataka watendaji hao  kusikiliza kwa makini na kuyapokea mafunzo hayo ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi

Nao washiriki wa mafunzo hayo wameshukuru kupatiwa  elimu hiyo  kwani itawasaidia katika utendaji wa kazi zao.

Aidha wameaahidi kuyafanyia kazi mafunzo waliyopatiwa ili kuimarisha afya za wananchi 

Hata hivyo wamesea  kuwa kupitia mafunzo hayo watahakikisha kuwa kazi zao zinafanyika kwa ufasnisi na   kwa haraka 

Mafunzo hayo ni ya Siku mbili na  yamewashirikisha  wakuu wa bodi ya Mfuko pamoja, watendaji na Uongozi