Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi  akimpa mkono Nd.Hamadi Matar Abdalla 39yrs Mkaazi wa Kinuni Magharibi “B” akiwa ni miongoni mwa  majeruhi wa ajali ya kuporomoka kwa Jengo la Nyumba ya Kihistoria ya Beit el Ajab juzi ambae amelazwa  katika Wodi ya wagonjwa mbali mbali  katika Hospitali ya Mnazi Mmoja alipowatembelea Wagonjwa waliolazwa katika haospitali hiyo leo (kulia kwa Rais)Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Dk.Marijani Msafiri Marijani.[Picha na Ikulu] 26/12/2020.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi  (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Dr.Riffat Kh.Juma (kulia) yanayomhusu  Nd.Hamadi Matar Abdalla 39yrs Mkaazi wa Kinuni Magharibi “B” akiwa ni miongoni mwa  majeruhi wa ajali ya kuporomoka kwa Jengo la Nyumba ya Kihistoria ya Beit el Ajab   alipofika  kuwaangalia wagonjwa katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmoja leo  (kushoto) Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Dk.Marijani Msafiri Marijani .[Picha na Ikulu] 26/12/2020.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi  (kushoto) akimuuliza hali Nd.Gharibu Juma (14yrs) mkaazi wa Kijichi Magharibi”A”akiwa katika Wodi Namba 1 ya wagonjwa mbali mbali  katika Hospitali ya Mnazi Mmoja alipowatembelea Wagonjwa waliolazwa katika haospitali hiyo leo.[Picha na Ikulu] 26/12/2020.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Dk.Marijani Msafiri Marijani   alipowasili  Hospitali Kuu ya Mnazo Mmoja leo kuwaangalia majeruhi wa ajali ya kuporomoka kwa Jengo la Nyumba ya Kihistoria ya Beit el Ajab jana.[Picha na Ikulu] 26/12/2020.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali na Kaimu Waziri wa  Afya na Ustawi wa Jamii Mhe.Simai Mohamed Said   alipowasili Hospitali Kuu ya Mnazo Mmoja leo kuwaangalia majeruhi wa ajali ya kuporomoka kwa Jengo la Nyumba ya Kihistoria ya Beit el Ajab juzi.[Picha na Ikulu] 26/12/2020.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi  (katikati) akimuangalia Nd.Haji Juma Haji (24yrs) aliyepata athari katika Inni akiwa ni miongoni mwa majeruhi 4 wa ajali ya kuporomokewa  na Jengo la Nyumba ya Kihistoria ya Beit el Ajab jana akiwa chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) Hospitali ya Mnazi Mmoja (kushoto)Mkuu wa Wodi ya Wagonjwa mahtuti Dk. Salum Shaaban Salum .[Picha na Ikulu] 26/12/2020. Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi  (kulia) akimuangalia Nd.Zamir Suleiman Salum (45yrs) aliyeumia Kifua akiwa ni miongoni mwa majeruhi 4 wa ajali ya kuporomokewa  na Jengo la Nyumba ya Kihistoria ya Beit el Ajab jana akiwa chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) Hospitali ya Mnazi Mmoja (katikati) Mkuu wa Wodi ya Wagonjwa mahtuti Dk. Salum Shaaban Salum.[Picha na Ikulu] 26/12/2020.