MABINGWA watetezi, Bayern Munich wamejihakikishia kwenda Hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya RB Salzburg katika mchezo wa Kundi A usiku wa jana Uwanja wa Allianz Arena Jijini Munich. Mabao ya Bayern Munich yalifungwa na Robert Lewandowski dakika ya 42, Maximilian Wober aliyejifunga dakika ya 52 na Leroy Sane dakika ya 68, wakati la RB Salzburg lilifungwa na Mergim Berisha dakika ya 73. Bayern Munich inafikisha pointi 12 na kuendelea kuongoza kundi hilo kwa pointi saba zaidi ya Atletico Madrid, wakati RB Salzburg inaendelea kushika mkia kwa pointi yake mmoja, nyuma ya Lokomotiv Moscow yenye pointi tatu kuelekea mechi za mwisho PICHA ZAIDI SOMA HAPA
BAYERN MUNICH YATINGA 16 BORA YAICHAPA 3-1 RB SALZBURG LIGI YA MABINGWA
By Alex Sonna
November 26, 2020 | 6:05 am

Related Stories
View all
Michezo
21 hours ago
TRA DODOMA YAADHIMISHA MIAKA 30 KWA MATEMBEZI YA HISANI, BONANZA
DODOMA, 27 Juni 2026 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Dodoma imefanya Matembezi ya Hisani pamoja na Bonanza la Michezo ikiwa ni sehemu…
Michezo
1 day ago
SENEGAL YAFUFUA MATUMAINI YA KUTINGA HATUA YA 32 BORA KOMBE LA DUNIA 2026
Timu ya Taifa ya Senegal imefufua matumaini ya kutinga hatua ya 32 Bora ya Kombe la Dunia 2026 baada ya kuichapa Iraq mabao 5-0…
