Waziri wa Nchi – Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akitoa neno la ufunguzi wakati wa mkutano wake na wawekezaji kutoka Marekani waliopo nchini alipokutana nao 17 Juni, 2019 katika Ukumbi wa Mikutano wa Hyatt Jijini Dar es Salaam ili kujadili masuala ya uwekezaji nchini.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Bw. Geoffrey Mwambe akiwasilisha mada ya masuala ya Uwekezaji nchini wakati wa kongamano hilo.
Waziri wa Nchi – Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki (katikati mwenye kitenge cha kijani) pamoja na Kaimu Balozi wa Marekani Nchini Dkt. Inmi Patterson (mwenye koti jeupe) wakifuatilia uwasilishwaji wa mada wakati wa kongamano hilo.
Waziri wa Nchi – Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki (mb) akizungumza na Kaimu Balozi wa Marekani Nchini Dkt. Inmi Patterson mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa Mikutano wa Hyatt Jijini Dar es Salaam walipokutana kujadili masuala ya uwekezaji nchini wa kwanza kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.
Waziri wa Nchi – Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji) Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza na waandishi wa habari masuala ua uwekezaji walipokutana nao wakati wa kongamano la kujadili masuala hayo kwa wawekezaji wa Kimarekani, kulia kwake ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.na kushoto kwake ni Kaimu Balozi wa Marekani Nchini Dkt. Inmi Patterson.



(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)