Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome kulia akiwa wilayani Maswa mkoani Simiyu akiangalia nyaraka za Bibi Kang’wa Kija ambaye ni msimamizi was mirathi ya Kija Gogadi aliekuwa akihitaji msaada wa sheria baada ya suala hilo kuchukua muda mrefu bila ya kumalizika.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome alievaa tai akisikiliza suala la Bibi Kang’wa Kija kutoka kwa mwanasheria wilayani Maswa ili kumsaidia mwananchi huyo ambaye ni msimamizi wa mirathi ya Kija Gogadi ambaye suala lake limechukua muda mrefu bila ya kumalizika.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akipokea nakala ya Taarifa ya utendaji kutoka kwa Msaidizi wa Sheria kutoka wilaya ya Itilima mkoani Simiyu alipozungumza nao mjini Bariadi Mkoani Simiyu.
WASAIDIZI wa sheria kutoka kituo cha msaada wa sheria wilayani Maswa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome na Msajili wa Watoa msaada wa sheria nchini walipokitembelea kituo hicho wilayani Maswa mkoani Simiyu
WASAIDIZI wa sheria kutoka wilaya za Maswa,Itilima na Meatu katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome na Msajili wa Watoa Msaada wa Sheria nchini walipokutana na wasaidizi wa sheria wa Mkoa wa Simiyu mjini Bariadi.
………………………..
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome ametoa huduma ya msaada wa sheria wilayani Maswa mkoani Simiyu.
Prof. Mchome amemhudumia mwananchi Kang’wa Kija aliyemkuta kaika kituo cha Msaada wa sheria wilayani Maswa.




